Nini dhambi kwa mwenye dhiki?

4 views

Lyrics

All my people
 East Africa
 Tanzania, Uganda and Kenya
 Dar es Salaam, A town
 Wherever you are
 Piga magoti, tuombe Mungu Hii ni siasa, dini, vita, ubwana,
 utwana, au kiama ghalika,
 sodoma na gomora?
 Simama imara, zunguka kila
 kona, kila anga angaza
 Kushoto, kulia, mbele, nyuma kote pitia
 Na hapo ulipojishikiza
 g'ang'ania, sikilizia, vumilia
 baadae usije jutia Hii ni mahususi na maalum
 kwa watu wangu
 Walemavu, vipofu, zeruzeru na
 wendawazimu
 Watoto wa mitaani, fukara,
 masikini na wenye akili zao timamu
 Hii kamba ngumu
 Mjue tunavutana na wenye
 nguvu
 Vitambi na mashavu
 Hakuna tena fair game Refarii kauzu
 Uwanja wenyewe mkavu
 Ujira mgumu, malipo finyu
 Kilichobaki kucheza rafu
 Tumechoshwa na ukabaila,
 ubepari na ubeberu
 Wakati ndo huu
 Ukombozi ndo huu
 Na sasa naamuru mliopo chini
 wote mpate divai ya vinibu
 Mtetezi wenu nikaze gidamu
 Nimwage sumu ya ----- juu yao
 Wajikune bila aibu
 Kwanza saluti kwa
 waliyotangulia kuzimu
 Pili tuombe Mungu
 Baba yetu, utupe mkate wetu wa kila siku
 Utujaze nguvu
 Tupate kudumu ndani ya game
 Tutakapofika kuzimu siku ya
 hukumu
 Utupe nafasi tupate kutubu Kwani tunajua tunatenda
 maovu
 Tunakula haramu
 Tunatumia kila mbinu
 Juju, uhalifu, upanganyifu
 Ili tuweze kujikimu Lakini isiwe kisingizio kwa
 wanadamu wengine
 kunyimwa haki zetu
 Kutuzibia riziki zetu
 Kutuita makafiri, dharau na
 kutukashifu Kwani nini dhambi
 Nini dhambi kwa mwenye
 dhiki,
 Kipi haram, kipi halali,
 Kila mmoja anaitaka hii riziki
 Kitendawili, vurugu mechi Huwezi tabiri Kwa nini?
 Uliza swali, kama
 sote tungekuwa wasomi,
 matajiri
 Ni nani angelifanya kazi za
 kutisha na hatari mfano ya
 mochwari Kila mmoja wetu hapa mjini
 kaja kwa dili
 Kila kitu, kila mahali
 Na hata ngozi ya mtu dili
 Wengine wachawi, waganga
 feki Matapeli, wasafiri ------
 Wakati wengine wapole kama
 walokole
 Mchana pirika nyingi maofisini
 Kumbe night kali, kahaba
 Shuga, jambazi, mengine ya kusitiri
 Ah!
 Wapo waliopoteza maisha
 katika kufight life
 Kumbukumbu zao zimebaki
 makaburini Na wapo waliopoteza kabisa
 tumaini la kuwini
 Hao roho zao utadhani
 wamezitoa rehani
 Wakikutight mahali fulani
 Inabidi uwakabidhi mshahara wote wa mwisho wa mwezi
 ()
 Kweli Bongo kutafuta braza
 Utajajuta utakapojikuta huna
 hata bukta
 Shauri yako we tegesha tu
 kama golikipa
 Na hao unaowategemea mwishowe watakutosa
 Huna elimu, hun fani
 Lakini nguvu, hulimi, uchumi
 unao unaukalia
 Kumbuka
 Kupata au kukosa yote ni kawaida
 Sometimes unalala unaota
 unakula
 Unakunywa, unapiga denda
 Na kula uroda na demu bomba
 Ukikurupuka tu unakuta patupu
 Hakuna kitu
 (, Yamat singing a
 traditional Maasai song)

Audio Features

Song Details

Duration
04:37
Key
5
Tempo
90 BPM

Share

More Songs by X Plastaz

Albums by X Plastaz

Similar Songs